Wednesday, May 8, 2013

HATIMA YA LWAKATARE NA ZOMBE KUJULIKANA LEO.

Wakati Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam ikitarajiwa kutoa uamuzi wa maombi ya Mkurugenzi wa Ulinzi na Usalama wa Chadema, Wilfred Lwakatare leo, pia itasikiliza rufaa ya kesi dhidi ya aliyekuwa Mkuu wa Upelelezi Mkoa wa Dar es Salaam (RCO), Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP), Abdallah Zombe.
Lwakatare na mwenzake, Ludovick Rwezahula Joseph wanakabiliwa na kesi ya ugaidi, walipandishwa kizimbani katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Machi 18 na kusomewa mashtaka manne yakiwamo ya ugaidi.
Taarifa zilizopatikana jana kutoka Mahakama Kuu na kuthibishwa na mmoja wa mawakili wanaomtetea Lwakatare, zilisema uamuzi wa maombi hayo utatolewa na Jaji Lawrence Kaduri leo saa 3:00 asubuhi.
Kuhusu Zombe, Mahakama Kuu itaamua ama kutupiliwa mbali, au kuendelea na usikilizwaji wa kesi hiyo.
Zombe alikatiwa rufaa na Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) akipinga hukumu ya Mahakama Kuu iliyomwachia huru Zombe na wenzake katika kesi ya mauaji ya wafanyabiashara wa madini kutoka Mahenge, mkoani Morogoro na dereva teksi wa Manzese, Dar es Salaam.


Chanzo:CHADEMA social media.

No comments:

Post a Comment

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...