Tuesday, April 30, 2013

HOTUBA YA MSEMAJI MKUU WA KAMBI RASMI YA UPINZANI BUNGENI MCH.PETER MSIGWA JUU YA MALIASILI NA UTALII.

Mchugaji Peter Msigwa.

HOTUBA YA MSEMAJI MKUU WA KAMBI RASMI YA UPINZANI MHE. MCHUNGAJI PETER MSIGWA, (MB) WIZARA YA MALIASILI NA UTALII, KUHUSU MAKADIRIO YA MATUMIZI KWA MWAKA WA FEDHA 2013/2014. (Yanatolewa chini ya Kanuni ya 99(9) toleo la mwaka 2013)



1.0 UTANGULIZI.
Mheshimiwa Spika,dhima kuu ya wizara hii ni uhifadhi endelevu wa maliasili na malikale na kuendeleza utalii kwa manufaa ya kizazi kijacho. Katika kufanikisha dhima hii wizara ina idara za wanyamapori, utalii, mambo ya kale, utawala na usimamizi wa rasilimali watu na sera na mipango, pamoja na taasisi, vyuo na wakala na mifuko ya uhifadhi inayosimamiwa chini ya wizara hii. Hotuba yangu imelenga kupitia changamoto mbalimbali ambazo zinaikabili wizara pamoja na kutoa mapendekezo mbalimbali. 

Mheshimiwa Spika, sisi kama wabunge bila kujali CHADEMA, CUF,TLP,UDP CCM au NCCR MAGEUZI tunaamini kwa dhati tunajua kipi ni chema kwa watu wetu na kwa ujumla kushawishika katika uendelevu wa maliasili zetu, haya hayawezi kufikia kwa kutetea maslahi ya sisi binafsi na vyama vyetu pasipo kujifanya kuingiwa na upofu na kutenda kile tunachokiamini. 

UTEKELEZAJI WA BAJETI YA 2012/2013 

Mheshimiwa Spika,Taarifa za wizara juu ya utekelezaji wa bajeti ya 2012/2013 mbele ya kamati na vile zinavyoonekana katika randama ya mapato na matumizi, inaonesha wazi jinsi wizara na serikali ilivyoweka nyuma swala la miradi ya maendeleo na ulinzi wa rasilimali asili za kitanzania hasa kwa manufaa ya Taifa. 

Mheshimiwa Spika, katika bajeti ya mwaka 2012/2013 bunge lilipitisha na kuidhinisha fedha za miradi ya maendeleo kutoka katika mapato ya ndani na nje, na hadi kufikia February 2013 wizara ili pokea sehemu ya fedha za nje tuu na hakuna fedha za ndani zilizoelekezwa katika miradi ya maendeleo, pamoja na kupata fedha za nje ambazo ni shilingi 360,002,100 kati ya shilingi 12,712,682,390 bado fedha hizo zilizopokelewa na wizara zinajumuisha fedha za mwaka 2011/2012 shilingi 3,288,835,448/- huu ni uthibitisho dhahiri wa serikali kutoweka kipaumbele miradi ya maendeleo na kuweka rehani kwa wahisani swala la kuendeleza Taifa.

Mheshimiwa Spika,Pamoja na wizara kutoa taarifa imeainisha changamoto zilizopo katika utekelezaji ikiwa ni pamoja na kukabiliana na ujangili,uhaba wa fedha, viendea kazi hafifu, je changamoto kuelezea chanagamoto hizi kwa serikali inayotangaza kukabiliana na tatizo la ujangili pasipo kutenga fedha za kuiwezesha wizara ni nia ya dhati kwa serikali kudhibiti ujangili unaofanywa na mitandao yenye kutumia fedha nyingi? 

Mheshimiwa Spika, katika miradi saba iliyopangwa kutekelezwa na wizara ni pamoja na miradi ya idara ya wanyamapori na idara ya misitu na nyuki kama ilivyoanishwa katika kasma namba 2001 na 3001, na serikali kutoipatia wizara fedha za ndani mpaka sasa ni dhahiri serikali kutotambua na kutoona wazi tatizo la ujangili na uharibifu wa misitu katika nchi yetu, Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni inaitaka serikali kupitia ahadi zake za kutokomeza ujangili ni vema sasa ikatekeleza kwa vitendo, hivyo basi hatuwezi tegemea wahisani kulinda rasilimali zetu huku taarifa kuonesha uhusikaji mkubwa wa mitandao ya ujangili kutoka nje ya nchi.

HISTORIA YA UHIFADHI KATIKA JAMII ZA WAFUGAJI


Mheshimiwa Spika, uhifadhi wa wanyamapori katika historia tangu utawala wa kikoloni sera na sheria zilizotumika kwa miaka mingi hususani maeneo ya hifadhi ya Ngorongoro, mfumo uliopo sasa pamoja na kutishia mustakabali wa wanyamapori nchini pia umekuwa ikidhoofisha usalama wa nchi na umiliki wa rasilimali za wafugaji wa Kimasai.

Mheshimiwa Spika, taasisi za uhifadhi wa wanyamapori zilizoongozwa kwa misingi ya kikoloni, hazikumtenganisha mtu kutoka katika mazingira yake ya asili, kwa kutozingatia yale yaliofanywa na Serikali za kikoloni katika hifadhi hizi mambo ya ulinzi dhidi ya mtu kutozingatiwa na kusababisha binadamu kutengwa na makazi yao moja kwa moja hususani jamii za kimasai katika maeneo ya Ngorongoro na raslimali zao za asili kuchukuliwa na wao kuachwa pasipo kupewa ardhi mbadala kwa matumizi ya shughuli zao za ufugaji.

Mheshimiwa Spika,wakati hoja ya kuundwa kwa maeneo ya hifadhi kama vile Eneo la hifadhi ya Ngorongoro (NCA) kipindi cha utawala wa kikoloni ni dhahiri serikali ya kikoloni ilipata kigugumizi cha kufanya maamuzi ya kutowashirikisha wamasai katika mchakato,lakini waliweza kuwashirikisha wanajamii ya kimasai na kuamua kwa pamoja juu ya uanzishwaji wa eneo la hifadhi pasipo kuwepo malumbano na serikali ya kikoloni, hivyo tofauti tunayoiona sasa ni jinsi serikali ya kikoloni ilivyotii na kuheshimu jamii za kimasai na kuwaacha wakiendelea na maisha yao. 


BOFYA READ MORE KUENDELEA

Monday, April 29, 2013

ZITTO KABWE ASIGINA BAJETI YA WIZARA YA MAJI ILIYOONGEZEWA BIL.184.5

Baada ya bajeti ya Wizara ya maji kuongezewa kiasi cha Tsh.bilioni 184.5 kama ilivyokuwa imeshauriwa na kamati ya bunge hapo awali,bado mgawanyo wa kifedha kwenye bajeti hiyo umeonekana kutokuwa na usawa kulingana na mgawanyo wa watu kati ya mijini na vijijini.
Mbunge wa Kigoma Kasikazini Mh.Zitto Kabwe (CHADEMA) ametoa muhtasari wa mgawanyo wa kifedha katika bajeti hiyo katika ukurasa wake wa mtandao wa kijamii kama ifuatavyo:- 
"Maji Bajeti yake ya 2013/14 licha ya nyongeza ya tshs 184.5 bilioni, bado mgawanyo wa Bajeti ya Maji umeegemea sana mijini. Kabla ya nyongeza ya bajeti, miradi ya mijini ilikuwa imepangiwa tshs 254bn wakati miradi ya vijijini ilipangiwa tshs 75bn tu. Baada ya kelele za Wabunge, miradi ya vijijini imepangiwa tshs 237bn wakati mijini imepanda mpaka tshs 266bn. Watanzania 74% wanaishi vijijini, lakini mgawo mkubwa unakwenda mijini. Lazima sasa tuweke uwiano wa mgawo wa rasilimali za kibajeti kulingana na wapi wapo Watanzania wengi. Watu wa vijijini wanaminywa sana. Mwalimu aliwahi kuonya kuwa "tusisahau maendeleo ya vijiji" tusiruhusu miji kunyonya vijiji kimaendeleo."

WATU 19 WAUAWA IRAQ

Bendera ya Iraq.
Watu 19 wameuwa na wengine kadhaa wamejeruhiwa baada ya mabomu matatu ya kutegwa kwenye gari kuripuka leo kwenye miji miwili ya Iraq, yenye wakaazi wengi wa waumini wa Kiislamu wa madhehebu ya Kishia.
Shambulio hilo limetokea kwenye miji ya Amarah na Diwaniyah, huku kukiwa na mfululizo wa ghasia za kidini kufuatia mapigano kwenye kambi ya Waislamu wa madhehebu ya Suni, kaskazini mwa Iraq.
Ghasia za kimadhehebu, zimeongezeka tangu Jumanne iliyopita, wakati vikosi vya usalama vilipojaribu kuwakamata waandamanaji katika kambi ya Waislamu wa madhdhebu ya Sunni kwenye mji wa Hawija. Hatua hiyo ilisabisha mauaji ya watu 32, wakiwemo wanajeshi watatu. Hakuna kundi lolote ambalo limedai kuhusika na mashambulio ya leo.

Chanzo: Idhaa ya Kiswahili ya Ujerumani

JOB VACANCIES- EAST AFRICAN COMMUNITY.

BOFYA HAPA KUPATA MAELEZO YA NAFASI ZA KAZI
Nafasi za kazi zifuatazo zimetangazwa:-

Principal Health Officer,

Senior e-Health & Informatics Officer,

National Open Health Initiative Officer,

Health Statistics & Data Management Assistant,

Programme Officer,

Monitoring & Evaluation Officer,

Knowledge Management & Communications Officer,

Programme Accountant,

Programme Administrative Assistant 


 



JACOB ZUMA AKUTANA NA TIANGAYE PRITORIA.

Rais Jacob Zuma wa Afrika Kusini na Waziri mkuu wa Jamhuri ya Afrika ya Kati, Nicolas Tiangaye, wamekutana mji mkuu wa Afrika Kusini, Pretoria, na wamekubaliana kuzidisha uhusiano baina ya nchi mbili hizo.
Uhusiano uliharibika baada ya wanajeshi 13 wa Afrika Kusini kuuwawa mwezi Machi wakati wapiganaji walipoiteka serikali ya Jamhuri ya Afrika ya Kati.
Vyombo vya habari vya Afrika Kusini viliarifu kuwa wanajeshi hao walipelekwa huko ili kampuni za biashara za Afrika Kusini zipate kandarasi za madini nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati.
Wakuu wa Afrika Kusini walikanusha hayo.

Chanzo: BBC

KIPANYA NA BODA BODA ZA BONGO

Saturday, April 27, 2013

DIAMOND AWASILI SALAMA UINGEREZA KWA AJILI YA SHOO.

Baada ya Msanii Nasibu maarufu Diamond kuwasili salama huko Uingereza tayari kwa shoo anayotarajia kuanza kuionyesha leo ameandika maneno yafuatayo kwenye mtandao wake wa kijamii:-
"Napenda kumshukuru mungu kwa siku ya leo....... Jumamosi mwanana.....nikiwa mbali na uso wa nyumbani, nikiwa ugenini kutafuta riziki......Shukrani za pekee pia kwenu mashabiki zangu wa dhati....mahana bila nyinyi si Mimi.....Nashukuru mungu kwa ulinzi wake... nipo salama salimini kwenye jiji la Malkia elizabeth....nashukuru uongozi mzima kwa  mapkezi mazuri na huduma nzuri mimi na dancers wngu.......!!

Nashukuru mungu kwa brekfast mwanana niliyopata na kunifanya nijiskie mwenye hari zaidi...kabla ya kuanza kukatiza mitaa ya jiji ili leye watu zaidi ya maelfu ya wanachi wanaotokea nchini mbalimbali duniani....!!"


Na hizi ndo picha mbali mbali za Diamond akiwa Ughaibuni hii leo.


Picha kwa hisani ya Mtandao wa kijamii wa Diamond.

NAFASI ZA KAZI WIZARA YA AFYA


                                            JAMHURI YA MUUNGANO TANZANIA
                                         WIZARA YA AFYA NA USTAWI WA JAMII
                                                            TANGAZO LA KAZI

Katibu Mkuu, Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii anapenda kuwatangazia nafasi za kazi kwa wote wenye taaluma za Kada za Afya ambao wako tayari kufanya kazi katika Utumishi wa Umma.
Vigezo na Masharti:
1. Awe ni raia wa Tanzania.
2. Awe na umri usiozidi miaka 45.
3. Watumishi wa Kada za Afya waliojiendeleza wakiwa kazini wasitume maombi bali waombe kwa waajiri wao kubadilishwa vyeo kulingana na sifa walizopata.
4. Watumishi ambao walikwishapangiwa vituo vya kazi miaka ya nyuma na hawakuripoti au kuacha kazi hawatapangiwa vituo vya kazi, kwa sababu hawataweza kuingia kwenye ‘Payroll’ ya Serikali.
5. Maombi yote yaambatanishwe na:- Nakala ya Cheti cha Taaluma, Nakala ya Cheti cha Kidato cha nne/sita, Maelezo binafsi (CV), Picha (Passport size mbili) za hivi karibuni, Nakala ya cheti cha usajili.
6. Vyeti vyote vya Taaluma na Kidato cha nne/sita ni lazima vithibitishwe na Hakimu au Wakili anayetambuliwa na Serikali.
7. Waombaji wanatakiwa kuchagua/kupendekeza maeneo matatu (Mikoa na Halmashauri) ambayo wangependa kupangiwa kazi kwa kuzingatia nafasi zilizoainishwa kwenye Kibali (Tazama Tovuti ya Wizara).
2
Waajiri wote wanatakiwa kuharakisha zoezi la kuwaajiri na kuwaingiza kwenye ‘Payroll’ ya Serikali wataalam wote watakaopangiwa vituo vya kazi kwenye mamlaka zao ikiwa ni pamoja na kuwalipa posho za kujikimu kwa wakati ili kuwaondolea usumbufu usio wa lazima watumishi husika.
Aidha, Waajiri wanakumbushwa kukagua na kuthibitisha uhalali wa vyeti vya kidato cha Nne na Sita vya wataalam hao kabla ya kuwaajiri.
Kwa utaratibu wa mwaka huu Katibu Mkuu Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, hatatoa barua za kupangiwa Vituo vya kazi. Majina ya watakaopangiwa vituo vya kazi yatatangazwa kwenye Tovuti ya Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii (www.moh.go.tz). Ukiona jina lako kwenye Tovuti au Gazeti nenda karipoti kwenye kituo ulichopangiwa kabla ya tarehe 25 Juni, 2013 ambako taratibu za ajira yako zitakamilishwa.
Maombi yote yatakayowasilishwa kwa mkono au barua pepe hayatafanyiwa kazi.
Barua zote zitumwe kwa njia ya posta kupitia anuani ifuatayo:-
Katibu Mkuu,
Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii,
S.L.P. 9083,
DAR ES SALAAM.

Mwisho wa kupokea barua za maombi ni tarehe 10 Mei, 2013.
Tangazo hili pamoja na mchanganuo wa nafasi za kazi vinapatikana katika tovuti ya Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii (www.moh.go.tz)

YANGA BAADA YA KUWA BINGWA WA LIGI KUU YAENDELEA NA MAZOEZI YA "GYM" KUIKABLI COASTAL UNION.

Pamoja na jana kutangazwa mabingwa wapya wa Ligi Kuu ya Vodacom msimu wa 2012/2013, kikosi cha timu ya Young Africans leo kimeendelea na mazoezi ya viungo na kujenga misuli (GYM) katika kituo cha mazoezi kilichopo jengo la Quality Cetntre kujiandaa na mchezo dhidi ya Coastal Union siku ya jumatano katika Uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam.
Young Africans ambayo jana imetangazwa rasmi kuwa Mabingwa wapya wa Ligi Kuu ya Vodacom 2012/2013 baada ya timu za Coastal Union na Azam FC kutoka sare ya bao 1-1, imeendelea kujifua kuhakikisha inamalizia mzunguko wa pili wa VPL kwa ushindi kama ilivyofanya tangu kuanza duru la pili.
Azam FC iliyokua na ndoto za kuweza kufikia pointi 56 za Yanga, ilikua ikiombea yenyewe kushinda michezo yake yote mitatu huku iikiombea Yanga kupoteza michezo yake miwili iliyosalia hali ambayo ilikwenda kinyume hapo jana kwa wauza mikate kupata sare ya 1-1 dhidi ya Coastal Union na kuifanya Yanga itangazwe mabingwa wapya wa VPL kwa kuwa na ponti 56 ponti 8 mbele ya Azam yenye pointi 48. 
Huu unakua ni Ubingwa wa 24 kwa Yanga tangu kuanzishwa kwa Ligi Kuu Tanzania bara rekodi ambayo hakuna timu yoyote inayokaribia kufuatia watani wa jadi Simba SC kuwa wametwaa ubingwa huo mara 18 tu.
Rekodi ya Ubingwa wa Yanga :1968, 1969, 1970, 1971, 1972, 1974, 1981, 1983, 1985, 1987, 1989, 1991, 1992,1993, 1996, 1997, 1998, 2002, 2005, 2006, 2007-2008, 2008-2009, 2010-2011, 2012-2013 
Baada ya kufanya mazoezi katika uwanja wa shule ya sekondari Loyola kwa siku tatu mfululizo kuanzia siku ya jumatano, jana wachezaji waliingia kambini katika hosteli za klabu zilizopo makao makuu mitaa ya Twiga/Jangwani kujiandaa na mchezo wa jumatano.
Kocha Mkuu wa Yanga mholanzi Ernie Brandts amekiongoza kikosi cha wachezaji 26 kufanya mazoezi ya gym leo katika kituo cha Quality Centre ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya mchezo unaofuata dhidi ya timu ya Coastal Union siku ya mei mosi jumatano  katika uwanja wa Taifa jijin Dar es salaam.
Yanga imebakisha michezo miwili (Costal Union 01.05.2013) na (Simba SC 18.05.2013) kabla ya kumalizika kwa Ligi Kuu ya Vodaom huku ikiwa tayari imeshatwaa Ubingwa mapema kabla ya kumalizika kwa Ligi Kuu ya Vodacom. 
Uongozi wa klabu ya Yanga unawaomba wanachama, wapenzi na washabiki wa timu ya Yanga kujitokeza kwa wingi siku ya jumatano (mei mosi) katika dimba la uwanja wa Taifa ili kuja kuwashangilia vijana wakiendeleza furaha ya kutwaa Ubingwa wa VPL msimu huu.
DAIMA MBELE, NYUMA MWIKO (DMNM)
EVER FORWARD, BACKWARD NEVER (EFBN) 

Chanzo: Mtandao wa kijamii wa Timu ya Yanga.

CHADEMA KUWASHA MOTO TABORA MJINI LEO,MNYIKA AMUANIKA NDUGAI KWA WAPIGA KURA WAKE.

Mh.Zitto Zuberi Kabwe.
Ikiwa ni katika muendelezo wa M4C na ufunguzi wa kanda ya magharibi, ambapo inatarajiwa kufanyika leo tarehe 27 Aprili 2013 ktk viwanja vya shule Town school karibu na kwa Papa Wemba Tabora mjini,Tayari viongozi wa kitaifa wameanza kuwasili usiku wa leo ambapo tayari Mhe. Zitto Kabwe ambaye ni mlezi wa kanda hiyo ameshawasili tayari kwa kuwasha moto wa kufa mtu leo ambapo tutakwenda kushuhudia Tabora kuwa kama Arusha kwa muamko kwani vijana wengi na wakazi wa hapo wana hamasa kubwa ya kufika ktk mkutano huo ili kukata kiu yao ya muda mrefu ya kukosa elimu ya uraia.

KUSHITAKIWA KWA NDUGAI.
 
Katika upande wa pili,Naibu Spika Mh.Jobu Ndugai ameshitakiwa kwa wapiga kura wake na Mbunge wa Jimbo la Ubungo na Kiongozi wa Kitaifa wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kwa kuwahoji iwapo walimtuma bungeni kufanya Ubabe wa  kuwatoa nje wabunge wenzie badala ya kuwatetea.
Mnyika alitoa Mashitaka hayo jana Aprilli 26, 2013 katika kijiji cha Iyegu, Kata ya Mlali, Wilaya ya Kongwa mkoani Dodoma, ambapo alisema amemkatia Rufaa Ndugai mara Tano bungeni bila majibu, kwa hiyo jana aliamua kumshitaki kwao ili wafanye maamuzi magumu juu ya mbunge wao asiyefanya kazi waliyomtuma.
Akizungumza katika Mkutano huo Mnyika alimshitaki Ndugai akiwahoji kama walimtuma kufanya hivyo, na waliposema Laa, aliwataka kufanya mabadiliko ya mwakilishi wa Jimbo lao kama wanataka kumaliziwa Kero zao zikiwepo Haki na Maendeleo ya kiuchumi na Matumizi bora ya Rasilimali zao.
Mwananchi mmoja alimhoji Mnyika “Je, ni nani aliyetayarisha, kulinda, kusimamia na kusafirisha Twiga wetu kwenda nje, lini watarejeshwa na waliohusika watafanywaje?.
Mnyika aliwajibu wananchi kwamba, wahusika wa usafirishaji wa Twiga wao ni vigogo walioko madarakani, na Twiga hao wako nchi mmoja ya Kiarabu, na mbali ya Twiga hao hivi karibuni Chadema itaibua suala la Tembo, na kuwaambia suluhisho la haraka kwa yote hayo ni kufanya mabadiliko ya viongozi mafisadi haraka.
Alipoulizwa Mauaji na Vitisho wanavyofanyiwa na Kundi linalojiita Kanyaga Twende, wanapoamua kujiunga na  vyama Upinzani, Mnyika aliwauliza kama wanayo simu ya Mbunge wao wamuulize ila wasimtukane, na waliposema hawana aliwatajia namba ya Ndugai na ya Mkurugenzi wa Usalama Chadema ambaye alidai atawawasaidia dhidi ya vitisho .
Aidha Mnyika kabla ya kushuka Jukwani saa 11.30 jioni, aliuuliza umati uliokuwepo uwanjani hapo, wangapi wapo tayari kwa mabadiliko ya M4C, watu wote karibu 1,000 walinyosha mikono na Mnyika akashuka kuelekea Kongwa kuungana na Mbunge wa Nyamagana, Ezekiel Wenje, kuendelea na Mikutano mingine.
 
Chanzo:Mtandao wa Kijamii wa CHADEMA.

Friday, April 26, 2013

8th EXHIBITIONS ON HIGHER EDUCATION , SCIENCE & TECHNOLOGY


THE TANZANIA COMMISSION FOR UNIVERSITIES
8th Exhibitions on Higher Education, Science and Technology
Diamond Jubilee Hall, Dar es Salaam
Wednesday 22th to Friday 24th May, 2013
The Tanzania Commission for Universities (TCU) wishes to inform all stakeholders and the general public that, the 8th exhibitions on Higher Education, Science and Technology will be held from 22nd-24th May 2013. These exhibitions are jointly organized by the TCU, the Ministry of Education and Vocational Training (MoEVT), Higher Education Institutions, as well as Regulatory, Professional and Research Bodies in and outside Tanzania.
Theme: "Building a knowledgeable, accountable and progressive society through Higher Education, Science and Technology"
Exhibitions’ Vision:
To become the leading national and regional state of the art exhibitions that promotes participation, enhances collaboration, builds up partnerships between higher education institutions and the Industry as well as developing mutual understanding on the issues that govern the quality of Higher education in the Country for the benefit of all humanity.
Exhibitions’ Mission:
To promote equity and collaboration, create partnerships and networks amongst the exhibitors and create linkages between higher education institutions, industry, research and development institutions and the market for national, regional and global socioeconomic development.
The Objectives of the Exhibitions:
o Creation of awareness among the general public about the development of Higher Education and Research Institutions and Professional Bodies in the country;
o Providing an opportunity to Higher Education Institutions to publicize their core functions and activities in the areas of teaching, research, consultancy as well as their current performance, potentials and future prospects;
o Providing a platform for Higher Learning and Research Institutions as well as Local and International Educational Business Companies to exchange ideas and experiences related to their core functions thereby triggering competition that will result in provision of quality higher education and research output;
o Enable the public and prospective applicants for admission into Higher Education Institutions within and outside Tanzania for the year 2013/2014 to interact with Universities, Regulatory Bodies and Research Institutions in order for them to make an informed choice;
o Sensitize the public on the application process through the Central Admission System (CAS).
Participants:
Exhibitors are Higher Learning and Research Institutions, Quality Assurance Regulatory Bodies and Foreign Universities from within and outside the East Africa Region. Local and International Educational Business companies are also invited to participate.
Exhibitions Venue:
The 8th exhibitions on Higher Education Science and Technology will take place at the Diamond Jubilee Hall, Dar es Salaam.
Duration:
The exhibitions will be open at 09.00 hours and close at 18.00 hours for three days from 22nd-24th May 2013.
Expected Outcome:
The exhibitions will enable the Government, employers and the general public to realize the opportunities available in Higher Education sector and in Educational Business Companies within and outside Tanzania and appreciate the critical roles they play in achieving national development goals.
Sponsorship:
We invite companies, Organizations and individuals who wish to sponsor the exhibitions. Upon some agreements, sponsors will be given a chance to advertise their business/ goods/services as well as a space to exhibit their business/ goods/services. Interested sponsors please contact the Office of Executive Secretary, TCU through below address.
Issued by the office of:
Executive Secretary,
Tanzania Commission for Universities,
Garden Road, Mikocheni,
P. O. Box 6562,
Tel: 22 2772657
Fax: 22 2772891
Email: es@tcu.go.tz
Dar es Salaam
You are all welcome

Source:TCU

KIPANYA ALIVYOSHEREHEKEA MUUNGANO LEO.

Naona mawazo yake ni sahihi na tuyafate ili tuendelee kuwa na amani na mshikamano.

BAADA YA AZAM KUBANWA MBAVU,HUU NDO MSIMAMO WA LIGI KUU YA VODACOM

 
Vodacom Premier League Ligi Kuu Ya Vodacom Msimu 2012/2013
Rank Teams Played Wins Draw Lost GD Points
1 Young Africans 24 17 5 2 31 56
2 Azam FC 24 14 6 4 22 48
3 Kagera Sugar 23 11 7 5 8 40
4 Simba SC 22 9 9 4 11 36
5 Mtibwa Sugar 24 9 9 6 3 36
6 Coastal Union 24 8 10 6 3 34
7 Ruvu Shooting 22 8 6 8 0 30
8 JKT Oljoro 24 7 7 10 -5 28
9 Prisons FC 24 6 8 10 -7 26
10 JKT Ruvu 24 7 5 12 -17 26
11 Mgambo Shooting 23 7 4 12 -7 25
12 Toto African 25 4 10 11 -12 22
13 Police M 23 3 10 10 -10 19
14 African Lyon 24 5 4 15 -20 19

CHADEMA WAFUNIKA NJOMBE,WANANCHI WAMKANA MAKINDA







Umati mkubwa uliohudhuria mkutano wa CHADEMA.
Katika hali ya kushangaza wakazi na wananchi wa Mkoa wa Njombe wamemkana Spika wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa madai kuwa hawakumtuma kutumikia chama bali kushughulikia kero na matatizo ya wananchi.

Hayo yalitokea katika mkutano wa hadhara uliofanyika mkoani hapo katikati ya Jimbo la Njombe Kusini ambalo yeye ndiye Mbunge wake.

Mkutano huo ambao uliongozwa na Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Mandeleo( CHADEMA), Dr wilbrod Peter Slaa,Naibu katibu mkuu kutoka zanzibari pamoja na wabunge machachari kutoka katika chama hicho(Mh Joseph Mbilinyi-Mbeya mjini, Mhezekiel Wenje-Nyamagana pamoja na Mchungaji Peter MsigwaIringa mjini) ambao wote kwa pamoja walifukuzwa bungeni kwa madai kuwa wanaleta fujo bungeni.

Dr .Slaa aliwataka wananchi wamthibitishie kuwa Makinda hakwenda bungeni kuwatetea bali kukitumikia Chama Cha Mapinduzi hivyo wabunge wa Chadema waendelee na kasi hiyo hiyo ya kuisimamia na kuikosoa serikali, hapo ndipo umati wote uliohudhuria mkutano huo uliponyoosha mikono yote juu kwa ishara ya kuunga mkono hoja iliyotolea na kiongozi huyo.

Spika Anne Makinda anatuhumiwa kwa kuliongoza Bunge ki ubabe hivyo kuwanyima wapinzani haki yao ya msingi ya kuihoji serikali juu ya matuimizi mabaya ya mali ya umma 



                               
Chanzo: Mtandao wa kijamii wa CHADEMA.

Breaking news:GODBLESS LEMA AMEKAMATWA NA POLISI NA KUWEKWA NDANI.

 Taarifa zilizotufikia hivi punde kutoka Arusha ni kuwa Mbunge wa Arusha Mjini amekamatwa na kuwekwa ndani kituo cha kati Arusha. Kukamatwa kwake ni baada ya mabishano ya muda mrefu nyumbani kwake na uvamizi wa Polisi wakati wa usiku  wa manane, lakini baadae Mh. Lema alikubali kukamatwa na kuchukuliwa na gari la polisi usiku na kupelekwa kituo kikuu cha polisi mjini Arusha.
Kukamatwa  kwake  kulikuja  baada  ya polisi  kuvunja mlango na kuingia ndani  na  kuendesha  msako  wa  nguvu  humo  ndani .Vitu  kama laptop, ipad, simu vipo mikononi mwa police.
 
Hata hivyo, wananchi wengi walijitokeza wakati mbunge wao anakamatwa ambo ambalo linaweza kusababisha uvunjifu wa amani mchana wa leo.

Habari zaidi zitawajia kadiri tutakavyokuwa tunazipata.

TAMKO LA MH. GODBLESS LEMA

Mh.Godbless Lema.
 
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Jana majira ya saa nne asubuhi nilipokea taarifa kutoka Chuo cha Uhasibu juu ya tukio la mauaji ya mwanafunzi yaliyotokea jana usiku kwa kuchomwa kisu eneo karibu na chuo , nilipita Chuoni hapo baada ya kusikia taarifa hiyo , nilikuta Wanafunzi wengi sana wakiwa wamekusanyika pamoja wakiwa na jazba huku Kamanda wa Jeshi la Polisi Wilaya akijaribu kuwasihi watulie wakati walipokuwa wanatafuta muafaka wa kuzuia jazba ambayo ilikuwa ina lengo la kuandamana kwenda kwa Mkuu wa Mkoa.

Nilipata faragha ya kuongea na Mwalimu aliyekuwa pale ( Dean of Student ) pamoja na OCD na wote walinieleza tatizo lilivyoanza na kuomba nitumie busara kuzuia jazba na maandamano hayo yaliyokuwa yamepangwa kuelekea kwa Mkuu wa Mkoa niliongea na wanafunzi na niliwasihi watulie na nilifanya jitihada za kumtafuta Mkuu wa Wilaya na Mkuu wa Mkoa na kwa bahati nzuri nilimpata Mkuu wa Mkoa na kumweleza juu ya kifo hicho na kile ambacho wanafunzi wanakusudia kufanya kuandamana kwenda ofisini kwake. Nilimuomba afike ili aweze kutuliza hali hile na pia atoe kauli juu ya tukio hilo baya la kuhuzunisha kwani ikizingatiwa kuwa ni zaidi ya mara moja matendo kama haya yamekuwa yakitokea na hakuna hatua zozote zimekuwa zikichukuliwa kuwahakikishia Wanafunzi Usalama wao na mali zao.

Mkuu wa Mkoa pamoja na mimi kumpa taarifa mapema aliahidi kufika mapema jambo ambalo halikufanyika na wanafunzi walianza kuwa wakali na nilifanya jitihada na hekima za hali ya juu kuvuta subira za wanafunzi hao ili Mkuu wa Mkoa afike . Baada ya Mkuu wa Mkoa kufika Makamu wa Chuo aliniomba niwaandae wanafunzi kumsikiliza Mkuu wa Mkoa na yeye alikwenda kumchukua Mkuu wa Mkoa na kumpa mukutasari wa tukio zima na hali halisi ya kilichokuwa kinaendelea na kimsingi Mkuu wa Mkoa alipofika Wanafunzi walitaka apande juu kuongea mahali ambako tulitumia kama jukwaa kwa maongezi wakati wote lakini badala yake mambo yafuatayo yalianza kutokea 

1) Mkuu wa Mkoa alikataa na kunitaka nishuke chini mahali alipokuwa yeye na timu yake ya ulinzi na usalama Mkoa kwa kweli nilitii na nilipotaka kuongea nae alinidharau na kuniambia hawezi kuongea na wanafunzi wahuni wasiokuwa na nidhamu maneno ambayo yaliwatia wanafunzi hasira zaidi na nilimsihi na kumuomba Mkuu wa Usalama wa Taifa Mkoa (RSO) kumshawishi Mkuu wa Mkoa kukubali kuongea nao kwani hali ilivyokuwa ni dhahiri kwamba wanafunzi wale walikuwa na jazba ya hali ya juu na hivyo hekima na unyenyekevu ndio ilikuwa njia pekee ya kutuliza hali hile. 

2) Mkuu wa Mkoa alitoa masharti kwamba asingeweza kuongea nao bila kipaza sauti na wanafunzi wote waende jengo lililokuwa karibu na Utawala na wakisha kaa atakuja kuongea nao jambo ambalo wanafunzi waligoma kwa imani kwamba jengo hilo lisengeweza kuchukua wanafunzi wengi na mimi niliaga naondoka kwenda msibani na wanafunzi waligoma nisiondoke mpaka watakapo sikilizwa na kwa kweli nilitii maombi baada ya kunizuia na kukaa mbele ya gari yangu.

3) Tulipokwenda eneo la kukutania na mara hii ilikuwa ni nje jirani ya jengo la utawala wanafunzi walikusanyika wakimsubiri Mkuu wa Mkoa na kabla hajafika nilitwa na yeye mwenyewe ili tuweke msimamo wa pamoja kama viongozi lakini badala yake alitumia Polisi kunitisha na kuhaidi kuwa nitamtambua kuwa yeye ni Serikali ,tulitofautiana tena nilipokataa hofu hiyo na ghafla tuliamua kwenda eneo la kuongea na wanafunzi na ndipo yafuatyo yalitokea “

Mkuu wa Mkoa wakati anaanza kuongea alianza kusema maneno yafuatayo “ Mnaona hiki Kifua na huu mwili wangu , na hapo ndipo hali ilipochafuka na kuamsha vurugu kubwa kutoka kwa Wanafunzi waliokerwa na kauli yake na Polisi wa walimchukua na tafrani kati ya Polisi na Wanafunzi ikapamba moto hali iliyosababisha mabomu ya machozi kulipuliwa kwa wingi kila kona ya chuo na kila mtu kuanza kukimbia kuangalia usalama wake nikiwemo mimi .
Nimesikiliza Mkutano wake na Waandishi wa Habari na leo nimesoma nakusikiliza vyombo mbali mbali vya habari kwamba ninatafutwa na Polisi kwa amri ya Mkuu wa Mkoa , nimeshangaa sana japo sio kumshangaa Mkuu huyu wa Mkoa kwani ufahamu na uwezo wake naujua ulivyo katika kufikiri na kutatua mambo ya msingi na muhimu , kwa jinsi nilivyomsikia na kumuona alivyokuwa anashughulikia tatizo lile lililotukutanisha jana pale Chuoni , kwa kweli nilishangazwa sana na kuogopa kama hekima ya Mkiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa angeweza kushughulikia tatizo lile kwa namna ile ya Kiburi , Dharau na Majivuno ambayo hakika ilikuwa ni chanzo cha wanafunzi kukataa kumsikiliza na ndipo alipoamua kuondoka huku zomea zomea ikiendelea kushamiri vizuri . Mabomu yalianza kupigwa , wanafunzi walipigwa na kunyang’anywa pesa , simu , na lap top na vitu mbali mbali ambavyo Polisi walikuwa wanaona vina thamani kwao , nilikuwa ninatazama mambo haya huku roho yangu ikiwa inauma sana kwamba wanaopaswa kulinda usalama wa raia na mali zao ghafla waligeuka kuwa vibaka wa kuumiza raia na kupora mali zao .

Ninawapa pole wanafunzi kwa msiba wa rafiki yao na siku ya jana ilikuwa ni siku ya Serikali kutumia busara kurudisha matumaini kwa wanafunzi wale pamoja na raia , lakini badala yake wafiwa walipotaka kudai haki zao za kulindwa , walipigwa , walidhalilishwa na Chuo chao kufungwa bila sababu ya msingi wala kuzingatia mambo muhimu .

Ifahamike kuwa Chuo cha Uhasibu Arusha kina wanafunzi kutoka sehemu mbalimbali za nchi hii, na amri ya mkuu wa mkoa kufunga chuo na kuamuru wanafunzi watawanyike ifikapo saa kumi na mbili jioni , huu ni ukosefu wa upendo , hekima , busara na utu ikizingatiwa kuwa sababu na mchochezi wa vurugu hizi ni Mkuu wa Mkoa kukosa maarifa na hekima.

Nimepokea ujumbe katika simu yangu kutoka kwenye simu yangu ya kiganjani kutoka kwa Mkuu wa Mkoa inayonitishia na kuweka maisha yangu kwenye hali ya hatari na ujumbe huo unasema “ UMERUKA KIHUNZI CHA KWANZA , NITAKUONYESHA KUWA MIMI NI SERIKALI ULIKOJIFICHA NITAKUPATA NA NITAKUPA KESI NINAYOTAKA MIMI “ Mwisho wa kunukuu .

Mwisho, Ninamshukuru kijana aliyerekodi tukio lote kuanzia mwanzo mpaka mwisho na hivi tutanza kusambaza video cd hizo Nchi ili watanzania wajue ukweli na Mh Rais aone utendaji mbovu wa wateule wake na vile nilitake Jeshi la Polisi kufanya kazi kwa kuzingatia sheria , maadili ,taratibu na kanuni za kazi na sio kuendesha Jeshi kwa matakwa ya kisiasa , kufanya hivi ni kuhatarisha usalama na utulivu wa Nchi yetu . 

“ Che Guavera alisema “ if you tremble indignation at every injustice then you are a comrade of mine “ 

Wanafunzi jipeni moyo bado kitambo kidogo Taifa hili litabadilika .


Godbless J Lema ( MP) 


25/4/2013.


Chanzo: Mtandao wa kijamii wa CHADEMA.

Thursday, April 25, 2013

UMOJA WA MATAIFA KUPIGA KURA JUU YA AZIMIO LA MALI


Baraza la usalama la Umoja wa Mataifa linatarajiwa kupigia kura azimio linalopendekeza kuundwa kwa kikosi cha kulinda amani nchini Mali.
Kikosi hicho chenye wanajeshi 12,600 kinajumuisha takriban wanajeshi 6,000 kutoka nchi za Magharibi mwa Afrika ambazo tayari zina wanajeshi wao nchini humo.
Azimio hilo limependekezwa na Ufaransa ambayo iliingilia kati mzozo wa Mali mnamo mwezi Januari ili kupambana na wapiganaji wa kiisilamu Kaskazini mwa nchi hiyo.
Kikosi hicho kinatarajiwa kwenda Mali mwanzoni mwa mwezi Julai kabla ya uchaguzi mkuu.
Hata hivyo duru zinasema kuwa azimio hilo limezua mjadala mkali.
Makundi ya kiisilamu yaliweza kutumia pengo la usalama lililotokea baada ya mapinduzi ya kijeshi mwaka jana na kuanza kushinikiza watu kufuata sheria za kiisilamu.
Miji iliyo Kaskazini mwa nchi, imeweza kudhibitiwa na jeshi la Ufaransa lakini baadhi ya wapiganaji wangali katika maficho yao.
Ufaransa ilianza kuondoa baadhi ya wanajeshi wake 4,000 mapema mwezi huu kutoka nchini humo, lakini imekuwa ikishinikiza Umoja wa Mataifa kupeleka wanajeshi wake.
Aidha wanajeshi wa Chad, wanasemekana kuwa wenye uzoefu mkubwa zaidi katika kupambana na wapiganaji jangwani, lakini nchi hiyo pia imeanza kuondoa wanajeshi wake kutoka Mali.
Sababu ya kikosi cha Umoja wa mataifa ni kulinda amani na kitakuwa na wanajeshi 11,200, pamoja na polisi 1,440.
Lengo lake kuu litakuwa kuweka uthibiti katika baadhi ya sehemu za Kaskazini mwa Mali ili kumaliza vitisho kutoka kwa wapiganaji wa kiisilamu.
Hata hivyo rasimu ya azimio hilo haisemi ikiwa wanajeshi hao wataweza kupigana na wapiganaji wa kiisilamu wenye uhusiano na kundi la al-Qaeda, lakini wanajeshi 1,000 wa Ufaransa,wataweza kusalia Mali.

Chanzo :BBC

KIPANYA LEO NA BUNGE LA TANZANIA

TAFAKARI,CHUKUA HATUA.

RAIS UHURU KENYATTA AZIDI KUTANGAZA BARAZA LA MAWAZIRI.

Rais wa Kenya, Uhuru Kenyatta
Rais wa Kenya, Uhuru Kenyatta ameendelea kulitangaza baraza lake la mawaziri. Katika uteuzi wa leo, Balozi Raychelle Omamo, ameteuliwa kuwa waziri wa ulinzi, huku Phylis Kandie akiteuliwa kuwa waziri wa uhusiano wa Afrika Mashariki na Utalii. Wengine walioteuliwa ni Charity Ngilu, ambaye atakuwa waziri mpya wa nyumba na makaazi, pamoja na Najib Balala, atakayekuwa waziri wa madini.Jumanne iliyopita, Rais Kenyatta, aliwateuwa mawaziri wanne, akiwemo Amina Mohamed, ambaye aliteuliwa kuwa waziri wa mambo ya nchi za nje na Henry Rotich, aliteuliwa kuwa waziri mpya wa Fedha. Wiki iliyopita Rais Kenyatta alielezea muundo wa baraza lake utakavyokuwa, kwa kulipunguza baraza hilo kutoka mawaziri 44 hadi kufikia 18.

CHANZO: IDHAA YA KISWAHILI YA UJERUMANI

SHEREHE ZA MUUNGANO ZAAHIRISHA MCHEZO WA SIMBA vs RUVU SHOOTING

TANGAZO
Mechi ya Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) kati ya Ruvu Shooting na Simba iliyokuwa ichezwe leo (Aprili 25 mwaka huu) Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam sasa itafanyika Mei 5 mwaka huu kwenye uwanja huo huo.
Mabadiliko hayo yametokana na Serikali kuutumia uwanja kwa ajili ya maandalizi ya sherehe za Muungano ambazo kitaifa zitafanyika kesho (Aprili 26 mwaka huu) Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) linawaomba radhi washabiki kwa usumbufu uliojitokeza kutokana na mabadiliko hayo na ghafla. Ratiba ya mechi nyingine za VPL zinabaki kama zilivyo.

Ligi hiyo inaendelea kesho (Aprili 26 mwaka huu) kwa mechi kati ya Coastal Union na Azam itakayochezwa Uwanja wa Mkwakwani jijini Tanga wakati Jumapili (Aprili 28 mwaka huu) itakuwa katika Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam ni Simba dhidi ya Polisi Morogoro.

Boniface Wambura
Ofisa Habari
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)

SERGIO RAMOSI ACHEZA MCHEZO WA 350 AKIWA NA REAL MADRID


Sargio Ramos akiwa anakabiliana na mchezaji wa Borrusia Dortmund katika mchezo wa jana Madrid
Beki wa kutumainiwa wa Real Madris Sergio Ramos akicheza mchezo wa jana akiwa na timu yake wakati wanacheza na Borrusia Dortimund amefikisha michezo 350 akiwa na Real madrid.
Jana akiwa mchezoni katika mchezo wa jana kama nahodha wa Real Madrid,ameandika historia hiyo katika maisha yake ya kisoka na takwimu zifuatazo zinafafanua zaidi:-
SERGIO RAMOS’ 350 MATCHES
Season League European Cup Copa del Rey Spanish Super Cup TOTAL
2005/06  33  7  6 -  46
2006/07  33  6  3 -  42
2007/08  33  7  3 2  45
2008/09  32  8  0 2  42
2009/10  33  7  0 -  40
2010/11  31  8  7 -  46
2011/12  34 11  4 2  51
2012/13  26  8  2 2  38
TOTAL 255 62 25 8 350

MAANDAMANO YATEKETEZA NYUMBA 20 LIWALE

Mh.Faith Mitambo Mbunge wa Liwale (CCM)
Takriban nyumba 20 zimeteketezwa katika maandamano yaliyofanywa na wakulima wa Korosho pamoja na waandamanaji wengine Kusini mwa Tanzania.Hii ni kwa mujibu wa mbunge mmoja wa eneo hilo.
Mbunge huyo, Faith Mitambo alisema kuwa majengo mawili nyumbani kwake mjini Liwale, yalichomwa na kuwa nyumba zingine mali ya baadhi ya wanachama wa chama tawala CCM ziliteketezwa.
Uharibifu huo ulianza baada ya wakulima kulipwa kiasi kidogo cha pesa ikilinganishwa na zile walizokuwa wamekubaliana kulipwa na serikali baada ya kuiuzia mazao yao mwaka jana.
Polisi zaidi wamepelekwa katika eneo hilo kuzuia ghasia zaidi.
Bi Mitambo, aliyekuwa mjini, Dodoma, wakati huo aliambia BBC kuwa alikuwa anazuru eneo bunge lake kudadisi hali ilivyo.
Alipokea habari kuwa waandamanaji waliokuwa wanajumuisha vijana , walianza kufanya fujo vijijini mnamo Jumanne asubuhi hadi walipofika mjini Liwale saa za jioni.
Mkaazi mmoja wa mji huo aliambia BBC kuwa mnamo Jumatano kulikuwa na hali ya wasiwasi mjini humo na kwamba polisi walikuwa wamewarushia gesi ya kutoa machozi wandamanaji ili kuwatawanya.
Maelfu ya wakulima wadogo wadogo wanaopanda Korosho nchini Tanzania na ambao huvuna mazao yao mwezi Oktoba, huyauza kwa mashirika mbali mbali kwa bei waliyokubaliana.
Mwandishi wa BBC mjini Dar es Salaam, Erick Nampesya anasema kuwa wakulima walikubaliana kulipwa shilingi 1,200 pesa za Tanzania kwa kila kilo ya korosho hizo.
Mwishoni mwa mwaka jana, wakulima walilipwa sehemu ya deni lao.
Lakini pale waakilishi kutoka kwa mashirika walipokwenda katika wilaya ya Liwale, kuwalipa sehemu ya mwisho ya deni lao, wakawa wamebadilisha makubaliano waliyokuwa wameafikiana.
Wakulima walilipwa nusu au chini ya nusu ya deni lililokuwa limesalia, baada ya kuambiwa kuwa bei ya Korosho ilikuwa imeshuka sana katika soko la kimataifa.
Wanasiasa wakuu ambao wakulima hao wanawalaumu kwa kukosa kuwasaidia ndio walikuwa wamewaelekezea ghadbabu zao
Wakulima wamekuwa wakilalamika kuhusu msukosuko wa bei za Korosho ambayo huathiriwa zaidi kulingana na msimu.
CHANZO : BBC

WATU 147 WAUWAWA KATIKA MKASA BANGLADESH

Maafisa nchini Bangladesh wamesema idadi ya waliofariki katika mkasa wa jengo kuporomoka imefikia 147 huku maafisa wa uokozi wakifanya kazi usiku kucha kutafuta watu waliokwama katika vifusi vya jengo hilo.Jengo hilo la orofa nane liliporomoka hapo jana asubuhi viungani mwa mji mkuu Dhaka katika eneo la Savar na inahofiwa mamia ya watu bado wamekwama chini ya vifusi vya jengo hilo lililokuwa na viwanda vya nguo.
Mashirika ya habari nchini humo yanaarifu kuwa watu waliripoti kuweko kwa nyufa kubwa katika jengo hilo siku moja kabla ya mkasa huo lakini wasimamizi wa jengo hilo inadaiwa hawakuchukua hatua zozote.Mkuu wa polisi katika eneo hilo Mohammed Asaduzzaman amesema polisi na baraza la mji huo wamewasilisha kesi tofauti dhidi ya mwenye jengo hilo kwa kutozingatia usalama.

CHANZO: IDHAA YA KISWAHILI YA UJERUMANI

CHADEMA WAITEKA MBEYA,WAMUONYA RAIS ASIIPIGIE DEBE CCM

Dr.Slaa akihutubia umati mkubwa katika mkutano jijini Mbeya.
  Katika kuendelea na ziara yao katika mikoa mbali mbali wabunge wa CHADEMA waliosimamishwa bungeni,jana wameendelea na ziara yao na kufanya mkutano mkubwa ulihudhuriwa na umati mkubwa wa watu mjini Mbeya.
Katika mkutano huo CHADEMA walimtahadharisha Rais kutokipigia debe Chama cha Mapinduzi.
 
Mbunge wa Mbeya Mjini Joseph Mbilinyi(Sugu) akihutubia mjini Mbeya.
Mbunge wa Mbeya mjini, Joseph Mbilinyi (Sugu) amemtahadharisha Rais Jakaya Kikwete asiitumie ziara yake ya Mkoa wa Mbeya kukipigia debe Chama Cha Mapinduzi(CCM) 
bali afanye kazi za kiserikali.
Rais Kikwete anatazamiwa kuwasili mkoani Mbeya, Jumapili ijayo kwa ziara ya kikazi ya siku nne.
Akizungumza katika mkutano wa hadhara jana Mjini Mbeya,Sugu alisema kuwa kitendo hicho kitasaidia kuimarisha umoja miongoni mwa wananchi wa Mbeya.
“Wakazi wa Mbeya muwe tayari kumpokea Rais Kikwete endapo ataifanya ziara yake kuwa ya kiserikali na yeye akiwa ni rais wa nchi na siyo kuifanya ziara hiyo kuwa ya kisiasa kwa vile tu yeye ni mwenyekiti wa CCM,”alisema Sugu.
Mkutano huo uliofanyika katika Uwanja wa Ruanda-Nzovwe, ulihudhuriwa pia na Katibu Mkuu wa Chadema,Dk Wilbroad Slaa, Mbunge wa Iringa, Mchungaji Peter Msigwa (Iringa mjini), Ezekiel Wenje(Mwanza mjini) na Highness Kiwia wa Jimbo la Ilemela. Sugu pia alitoa miezi mitatu kwa Halmashauri ya Jiji la Mbeya kuhakikisha Soko Jipya la Mwanjelwa linakamilika ifikapo Julai mwaka huu.

Alitishia iwapo kufikia muda huo halijakamilika yeye na wananchi wenzake watavamia soko hilo na kufanya kazi za ujenzi wenyewe.
Akizungumza katika mkutano huo, Mbunge wa Jimbo la Iringa mjini, Peter Msigwa alisema kuwa wamejipanga kufanya maamuzi magumu kama Spika wa Bunge, Anne Makinda
ataendelea kuwapendelea wabunge wa CCM.

Dk Willbroad Slaa alisema sababu ya wabunge wa Chadema kufukuzwa bungeni ni
kutokana na kutekeleza majukumu waliyotumwa na wananchi.
Aliwataka Wananchi kuendelea kuwaunga mkono na watambue kuwa CCM na Serikali yake inafanya kazi ya kutetea ubovu wa Serikali na kuwafanya Watanzania kuwa katika hali ya
umasikini huku walionacho wakizidi kuneemeka.

 
Wabunge wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) waliosimamishwa bungeni wiki iliyopita wameamua kwenda kuwashitaki Spika Anna Makinda na Naibu wake Job Ndugai kwa wananchi kwa njia ya kuitisha mikutano ya mihadhara.
Chanzo: Mtandao wa kijamii wa CHADEMA.
 

Wednesday, April 24, 2013

REAL MADRIL YATOTA UJERUMANI,YAPIGWA 4-1 NA BORRUSIA BOTMUND

 Timu ya Real Madrid  ya Hispania ikicheza katika mchezo wa nusu fainali ya pili imekumbana na dhahama ya kufungwa na Borrusia Dotmund goli 4 kwa 1. Matokeo haya yanatofautiana kidogo na yale waliyopata wahasimu wao wakuu Barcelona iliyofungwa 4-0 jana na Bayern Munchin.
Kwa matokeo haya,ili Real Madrid aweze kufuzu kucheza fainali katika mchezo wa marudiano utakaochezwa Hispania wanatakiwa washinde 3-0.

Timeline

soundEnable
Borussia Dortmund
Borussia Dortmund4 - 1Real Madrid
  • R. Lewandowski 8
  • R. Lewandowski 50
  • R. Lewandowski 55
  • R. Lewandowski 67 (P (penalty))
  • C. Ronaldo 43
Real Madrid
Borussia DortmundEvents
  • Goal: Robert Lewandowski 8min (minute symbol)
  • Goal: Robert Lewandowski 50min (minute symbol)
  • Goal: Robert Lewandowski 55min (minute symbol)
  • Penalty: Robert Lewandowski 67min (minute symbol)
  • Substitution: Sebastian Kehl (In) / Jakub Blaszczykowski (Out) 82min (minute symbol)
  • Substitution: Kevin Großkreutz (In) / Lukasz Piszczek (Out) 83min (minute symbol)
  • Substitution: Julian Schieber (In) / Ilkay Gündogan (Out) 90+2min (minute symbol)
  • Yellow Card: Robert Lewandowski 70min (minute symbol)
Real MadridEvents
  • Goal: Cristiano Ronaldo 43min (minute symbol)
  • Substitution: Karim Benzema (In) / Gonzalo Higuaín (Out) 68min (minute symbol)
  • Substitution: Ángel Di María (In) / Luka Modric (Out) 68min (minute symbol)
  • Substitution: Kaká (In) / Xabi Alonso (Out) 80min (minute symbol)
  • Yellow Card: Sami Khedira 54min (minute symbol)
  • Yellow Card: Mesut Özil 64min (minute symbol)
  • Yellow Card: Sergio Ramos 90+2min (minute symbol)
min (minute symbol)
Competition
Champions League
KO (kickoff)
24 Apr 2013 20:45
REF (referee)
Bjorn Kuipers
AT (venue)
Signal Iduna Park
FT (fulltime)

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...