Friday, May 31, 2013

HOTUBA YA MSEMAJI MKUU WA KAMBI RASMI YA UPINZANI BUNGENI MHE. SYLVESTER MHOJA KASULUMBAYI (MB) KUHUSU MAPITIO YA UTEKELEZAJI WA BAJETI YA MWAKA 2012/13 NA MAKADIRIO YA MATUMIZI YA WIZARA YA MAENDELEO YA MIFUGONA UVUVI KWA MWAKA WA FEDHA 2013/14 (Inatolewa chini ya Kanuni ya 99 (9), ya Kanuni za Kudumu za Bunge Toleo la Mwaka 2013)

A: UTANGULIZI
Mheshimiwa Spika, dira ya Wizara ya Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi ni kuhakikisha kuwa raslimali za mifugo na uvuvi zinaendelezwa na kutunzwa katika mazingira endelevu kwa ajili ya ukuaji wa uchumi na kuboresha maisha ya wananchi.  Aidha dira inalenga kuhamasisha ufugaji wa kisasa na uvuvi endelevu ili kujenga uchumi endelevu kwa jamii nzima ya wafugaji na wavuvi na taifa kwa jumla.
Mheshimiwa Spika, Licha ya ukweli kwamba wafugaji na wavuvi wana mchango mkubwa katika uchumi wetu, Serikali hii ya CCM imeshindwa kuwapatia maeneo maalum kwa ajili ya malisho kwa maendeleo ya mifugo yao. Wafugaji wamekuwa wakihamishwa na au wakifukuzwa kutoka eneo moja la nchi hadi eneo lingine kama vile hawana haki ya kufanya shughuli za kiuchumi kama ufugaji katika nchi yao. Ni aibu kwa  Serikali kushindwa kuwapatia wafugaji mahitaji muhimu ambayo yangepelekea ufugaji wao kuwa wa kisasa, kibiashara na endelevu kama ilivyobainisha katika dira ya Wizara hii.
Mheshimiwa Spika, Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni inayoongozwa na CHADEMA, haioni sababu ya Serikali kuwapatia wafugaji maeneo ya kufugia  kwa kuwa wafugaji wangeweza  kuingia ubia na mashamba makubwa ya mifugo ambayo yalikuwa yanamilikiwa na Ranchi za Taifa, lakini kutokana na ubinafsi na ufisadi uliofichwa kwenye kivuli cha cha sera ya ubinafsishaji,  Serikali ya CCM imesimamia zoezi la  viongozi wa serikali na Chama cha Mapinduzi wakigawiana ranchi hizo na kuwaacha wafugaji wakifukuzwa ovyo na kupewa jina la wachungaji.
Mheshimiwa Spika, kwa upande wa wavuvi hali ni hiyo hiyo,  kwani mapato mengi ya Serikali  yanayokusanywa kutoka katika sekta ya uvuvi yanatokana na wavuvi wadogo ambao mara zote wao ndio waathirika wa mfumo kandamizi wa Serikali.  Zana za uvuvi zinapokamatwa, wao ndio wanapata hasara, lakini wauzaji wa zana hizo za uvuvi  wala hawaulizwi na wala hakuna hatua zinazochukuliwa dhidi yao.
 Mheshimiwa Spika, changamoto kubwa inayozikabili sekta hizi za ufugaji na uvuvi ni kwamba sekta  zote mbili hazina bima dhidi ya  majanga ambayo yanaweza kutokea.  Katika mazingira kama haya, dhana ya kuwa sekta za kisasa, kibiashara na endelevu inakuwa ngumu sana.
Mheshimiwa Spika, katika hotuba ya Msemaji Mkuu wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni kwa mwaka wa fedha 2012/2013 liainisha mapungufu makubwa katika ya kiutendaji na kiuwajibikaji kwa wizara hii na kuitaka Serikali kufanya mambo yafuatayo:
1.      Kuwajibika kwa uzembe wa kuitelekeza meli ya uvuvi ya Tawariq iliyokamatwa ikifanya uvuvi haramu katika ukanda wa bahari ya hindi hadi meli hiyo kuharibika kabisa na kuanza kuzama bila faida yoyote?
2.      Kuchukua hatua dhidi ya mwekazaji wa Kagera Sugar kwa kushindwa kuendeleza shamba la ukubwa wa hekta 45,000 (sawa na ekari 112,500) kinyume na mkataba.
3.      Kueleza sababu za kuwapa mashamba makubwa wawekezaji wa kigeni na kuwanyanyapaa wafugaji wa asili kinyume cha sheria.
4.      Kutatua migogoro ya ardhi baina ya wakulima na wafugaji ambayo mara kadhaa imesababisha uvunjifu wa amani na umwagaji damu miongoni mwa wananchi.
5.      Kujenga viwanda vya kusindika nyama katika mikoa ya wafugaji ili kuongeza thamani ya bidhaa ya nyama na hivyo kukuza uchumi.
6.      Kuweka wazi kiasi cha fedha kinachopatika kama mrahaba kutokana na uvuvi katika bahari kuu, pamoja na fedha za leseni kwa meli zinazofanya uvuvi katika ukanda wa bahari kuu.


WANAFUNZI WALIOFANYA VIZURI ZAIDI KATIKA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE 2012.



BARAZA   LA MITIHANI  LA TANZANIA




WANAFUNZI WALIOFANYA VIZURI ZAIDI KATIKA MTIHANI WA CSEE 2012


 1. Watahiniwa Kumi (10) bora Kitaifa:

NAFASI
NAMBA
JINA
JINSI
JINA LA SHULE NA MKOA
1
S0189-0063
SAID JUMA IRANDO
M
FEZA BOYS'   S  S  (DAR ES SALAAM)
2
S4459-0028
ALEX  ELIFAS
M
JUDE MOSHONO   S   S  (ARUSHA)
3
S0189-0039
JASPER GEOPHREY KAJIRU
M
FEZA BOYS'   S  S   (DAR ES SALAAM)
4
S2549-0086
MOSES J BOSCO
M
ALPHA SECONDARY    S  S (DAR ES SALAAM)
5
S4213-0074
YOHANA L MAYENGA
M
MARIAN BOYS' S   S  (PWANI)
6
S0239-0072
NGUSE  NGULUMBI
F
ST. FRANCIS GIRLS   S   S  (MBEYA)
7
S4213-0044
JOSHUA Z AZZA
M
MARIAN BOYS'  S    S  (PWANI)
8
S0189-0062
SAID ATWAYA NCHIMBI
M
FEZA BOYS'   S  S   (DAR ES SALAAM)
9
S0867-0134
LUPYANA L KINYAMAGOHA
M
PANDAHILL   S   S  (MBEYA)
10
S0101-0350
PETER SEREKA KICHOGO
M
AZANIA    S   S  (DAR ES SALAAM)



2.    Wasichana Kumi (10) bora Kitaifa

NAFASI
NAMBA
JINA
JINA LA SHULE NA MKOA
1
S0239-0072
NGUSE  NGULUMBI
ST. FRANCIS GIRLS   S  S   (MBEYA)
2
S0239-0078
SAMMOTA  CHUNGU
ST. FRANCIS GIRLS   S   S  (MBEYA)
3
S0239-0075
RAHMA  MKWATA
ST. FRANCIS GIRLS   S    S (MBEYA)
4
S0239-0018
DIANA  MGAYA
ST. FRANCIS GIRLS  S  S  (MBEYA)
5
S1060-0066
REBECCA J MWAMBEGELE
ST.MARY'S   S   S (DAR ES SALAAM)
6
S0239-0010
BELDA  THOMAS
ST. FRANCIS GIRLS  S   S  (MBEYA)
7
S0239-0002
AGNES  NTAPARA
ST. FRANCIS GIRLS   S  S  (MBEYA)
8
S0248-0045
JOANGELINE J BAMWENZAKI
MARIAN GIRLS   S  S   (PWANI)
9
S0298-0011
FATMA M MOSHI
FEZA GIRLS' S  S   (DAR ES SALAAM)
10
S0239-0045
JESCA  CHENGULA
ST. FRANCIS GIRLS   S  S  (MBEYA)


3.      Wavulana Kumi (10) bora Kitaifa


NAFASI
NAMBA
JINA
JINA LA SHULE NA MKOA
1
S0189-0063
SAID JUMA IRANDO
FEZA BOYS'   S    S  (DAR ES SALAAM)
2
S4459-0028
ALEX  ELIFAS
JUDE MOSHONO   S  S   (ARUSHA)
3
S0189-0039
JASPER GEOPHREY KAJIRU
FEZA BOYS'S   S   S   (DAR ES SALAAM)
4
S2549-0086
MOSES J BOSCO
ALPHA   S   S    (DAR ES SALAAM)
5
S4213-0074
YOHANA L MAYENGA
MARIAN BOYS'   S  S   (PWANI)
6
S4213-0044
JOSHUA Z AZZA
MARIAN BOYS'   S   S   (PWANI)
7
S0189-0062
SAID ATWAYA NCHIMBI
FEZA BOYS'   S  S  (DAR ES SALAAM)
8
S0867-0134
LUPYANA L KINYAMAGOHA
PANDAHILL   S   S   (MBEYA)
9
S0101-0350
PETER SEREKA KICHOGO
AZANIA     S   S   (DAR ES SALAAM)
10
S0692-0065
NORBERT S KIMARYO
ROSMINI    S   S   (TANGA)

MATOKEO YA KIDATO CHA SITA 2013 HAYA HAPA.

MATOKEO YA KIDATO CHA SITA 2013

2013 Esmod Berlin Hessnatur Scholarships for International Masters Programme in Germany

Esmod Berlin International University of Art for Fashion funded Hessnatur Scholarships for the International Masters Programme – Sustainability in Fashion. Scholarships are provided in the field of fashion. Scholarships will cover half of the tuition to complete the innovative one-year English taught course. International Students can apply for these scholarships. Candidates should have a fashion background in design, marketing or similar and a strong interest in sustainability in fashion. The course start date is 17th October 2013. The application deadline is 30th June 2013.


MAREKEBISHO YA HOTUBA YA UPINZANI YA WIZARA YA MAMBO YA NJE.

Marekebisho ya hotuba ya upinzani ya Wizara ya Mambo ya Nje

Mabadiliko katika ukurasa wa 8 aya ya pili inayoanza na maneno ‘Mheshimiwa Spika, Kwa upande wa chama cha CUF....na kuishia na maneno…Israel Liberal ‘ sasa isomeke:
“Mheshimiwa Spika, kwa upande wa chama cha CUF, kutokana na itikadi zake za mrengo wa Kiliberali chama hicho ni mwanachama wa Umoja wa Vyama vya Kiliberali Duniani (Liberal International). Kwa mujibu wa tovuti ya umoja huo CUF imejiunga na Oxford Congress ya Liberal International Mwaka 1997.
Mwaka huo huo Liberal International ilitoa msimamo wa pamoja wa umoja huo uliotwa Liberal Manifesto (Ilani ya Kiliberali) ya 1997 iliyopitishwa katika mkutano mkuu wake wa 48 uliofanyika tarehe 27 mpaka 30 Novemba 1997 katika ukumbi wa Mji wa Oxford nchini Uingereza.
Katika ilani hiyo ya waliberali, umoja wa vyama hivyo ulikubaliana msimamo wa pamoja, nanukuu: “the extension of the rules of equality to sexual minorities and the recognition that homesexuality and lesbianism are legitimate expressions of personal proclivities”. Kwa Tafsiri rahisi waliberali hao walipitisha ajenda ya waliberali katika karne ya 21 (The Liberal Agenda in the 21st Century) ya kuutambua ushoga na usagaji kama matendo halali.
Hii ni kwa mujibu wa tangazo la Umoja huo kwenye mtandao wao wa waliberali ulimwenguni, likiungwa mkono na Waziri wa Haki na Usawa wa Uingereza, Lynn Featherstone kutoka chama cha Liberal Democrats wakati chama hicho(www.liberal-international.org)  kilipokuwa kinapitisha azimio la kuruhusu ndoa za jinsia moja kama haki ya mtu mmoja mmoja. Kupitia umoja hao CUF inashirikiana na vyama vingine kama vile LPC ya Canada, Det Radikale Venstre cha Norway, FDP cha Ujerumani, Israel Liberal………”
Ezekiah Dibogo Wenje
Msemaji wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa

                                                                        30 Mei 2013

Thursday, May 30, 2013

MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2012 HAYA HAPA.

MATOKEO YA KIDATO CHA NNE

MATUKIO KADHAA YA BAJETI YA WIZARA YA NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI 2013/2014.



MSc SCHOLARSHIP PROGRAM IN FRANCE, 2013.

International Space University is offering financial aid to MSc students to study in France. The scholarship covers tuition fees. Students from Europe, USA, Canada and developing countries are eligible to apply for this MSc scholarship. Scholarship is granted on the basis of academic and professional merit, financial need, and demonstrates effort in personal fund-raising. Application should be submitted online.

Study Subject(s): The scholarship is provided to study space studies at International Space University in France.
 

YANGA YAIKABIDHI MIL 25 NA TBL

Meneja wa Bia ya Kilimanjaro George Kavishe kushoto akimkabidhi mfano wa hundi Katibu Mkuu wa Young Africans Lawrence Mwalusako leo katika hafla iliyofanyika katika kiwanda cha bia TBL IIlala.
Kilimanjaro Premium Lager – wadhamini wakuu wa timu ya Yanga  imetoa kiasi cha shilingi milioni 25 kama zawadi kwa timu hiyo kwa kushinda Ligi Kuu ya Vodacom 2012/2013. 
 
Akikabidhi hundi ya Sh milioni 25 kwa Yanga SC, Meneja wa bia ya Kilimanjaro Premium Lager, George Kavishe alisema Kilimanjaro Premium Lager imefurahishwa sana na ushindi wa timu ya Yanga na kusema imejizatiti kikamilifu kuisaidia timu ambayo imeibuka bingwa katika ligi yenye ushindani mkubwa kutokana na kuibuka kwa timu mpya zenye nguvu.
    
“Yanga imekuwa ikicheza mpira mzuri kipindi chote cha msimu wa ligi kuu, na sio ajabu wao kuibuka washindi wa Ligi hii. Napenda kuwapongeza wachezaji wa Yanga, kocha na Uongozi mzima wa Yanga kwa  matokeo mazuri ya kushinda Ligi kuu kwa mara ya 24 sasa.”
 
Kavishe aliongeza kuwa zawadi hiyo ni sehemu ya sh bilioni 1.5 ya udhamini wa Kilimanjaro Premium Lager kwa Yanga   na imetolewa kwa lengo la kuhamasisha klabu kujitahidi kwa ushindi zaidi na kusaidia klabu katika maandalizi yake kwa ajili ya mashindano ya kimataifa ambayo tayari Yanga ina sifa za kushiriki kutokana na ubingwa waliojipatia.
 
Akipokea hundi hiyo, Katibu mkuu wa Yanga , Bwana Lawrence Mwalusako alisema Yanga inaishukuru sana Kilimanjaro Premium Lager kwa mchango wao. Aliongeza kuwa Yanga ni timu nzuri na yenye nguvu kutokana na uongozi imara pamoja na udhamini mkubwa kwa bia ya Kilimanjaro Premium Lager.  
 
‘‘Mafanikio yetu ya uwanjani ni kielelezo cha mafanikio ya kampuni na pia (TBL) na bia ya Kilimanjaro Premium Lager kwa ujumla ambayo imekuwa ikitusaidia sana. Kilimanjaro  Premium Lager imetoa mchango mkubwa sana katika kuipa timu msukumo uliopelekea mafanikio haya,’’ alisema Mwalusako.
 
Mwalusako aliongeza “Yanga sasa ina nafasi ya kuonekana kwenye jukwaa la kimataifa la soka kutokana na mafanikio haya’’.  “Tunaamini kuwa kutokana na udhamini wa Kilimanjaro Premium Lager tutaendelea kukua na kufanikiwa.’’
 
Yanga itawakilisha Tanzania katika michuano ya Klabu Bingwa Afrika na Kombe la Kagame.
MWISHO.

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...